Jumapili, 4 Mei 2014

2000, WASADIKIWA KUFA HUKO KASKAZINI, KASKAZINI MASHARIKI, NCHINI AFGHANISTAN.

Baadhi walipanda kwenye paa kusubiri msaada wa uokoaji

WATU wapatao 2000, wanasadikiwa kufa na wengine 4000, kupoteza makazi yao kutokana na maporomoko ya ardhi katika maeneo ya vijijini kwenye mkoa wa Bad khshan.

Vijiji hivyo vimefunikwa na udongo wenye ukubwa wa karibu mita 10, kwenda juu baada ya eneo la mlima mmoja kuporomoka kutokana na mvua kubwa zinazonyesha.

Miili ya watu wapatao 350 imepatikana katika maporomoko ya ardhi kaskazini mashariki mwa taifa hilo na hakuna mtu yoyote aliyepatikana akiwa hai.

Aidha, taarifa kutoka Umoja wa Mataifa (UN) zinasema karibu watu 4000 hawana makazi, ambapo juhudi za uokoji zinaendelea siku ya pili.


Mvua  zilizonyesha na kusababisha mafuriko na kuleta  madhara kwa wananchi wa Afghanstan

Ijumaa, 2 Mei 2014

WATU 19, WAMEUWA BAADA YA KUTOKEA MLIPUKO KATIKA MJI KUU WA NIGERIA, ABUJA.

Baadhi ya watu waliojeruhiwa katika mlipuko huo.
Mkurugenzi wa idara ya kushughulikia mikasa na hali ya dharura- FEMA- Abbas G Idriss, alisema watu 60 walijeruhiwa lakini sita kati yao wametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani, ambapo magari sita yameharibiwa katika mlipuko huo.

Mlipuko huo ulitokea katika eneo la Nyanya, karibu na kituo cha basi ambako zaidi ya watu 70 waliuwawa katika shambulizi la tarehe14 mwezi Aprili.

Waandishi wanasema kuwa mlipuko huo umesababishwa na bomu lililotegwa ndani ya gari. Mmoja wa walioshuhudia kisa hicho amesema aliona miili 20 ya watu waliouwawa.

Hakuna kundi lililodai kuhusika katika shambulizi hilo lakini kundi la wanamgambo wa kiislamu la Boko Haram limewahi kutekeleza mashambulizi kama hayo mjini Abuja

Mengi ya mashambulizi ya Boko Haram yamekuwa yakitokea katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria, lakini shambulizi la bomu la Aprili 14, lilizua hofu kwamba huenda wanamgambo hao wameanza kupanua maeneo wanayoendeleza harakati zao.

Alhamisi, 1 Mei 2014

WASICHANA 6000, MTWARA KUNUFAIKA NA MRADI WA HAKUNA WASICHOWEZA BAADA YA KUPATA ELIMU NA MISAADA YA VIFAA VYA KUJISITIRI WAKATI WA HEDHI.

Wasichana mkoani Mtwara wamenufaika na elimu ya afya pamoja na vifaa vitakavyowasaidia kujisitiri
wakati wa hedhi.

Elimu hiyo na msaada vimetolewa kupitia mradi wa ujulikanao Hakuna Wasichoweza unaotekelezwa na
asasi ya T-MARC Tanzania kwa ufadhili wa watu wa Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la Kimarekani
USAID kwa ushirikiano na Vodacom Foundation.

 Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo kwa wasichana walengwa wa mradi, Meneja wa Mradi wa huo, Doris Chalambo alisisitiza umuhimu wa kuwawezesha wasichana kama njia ya
uhakika ya kufanikisha maendeleo ya  jamii na Taifa.

 ‘’Awamu ya kwanza ya mradi huu imewafikiwa jumla ya wasichana 5000 katika shule za msingi za Mtwara na jumla ya wasichana 1000 walioko nje ya shule katika kata 17", alisema Doris.

Walengwa wa mradi huu ni wasichana wenye umri wa miaka 9 – 15. Jumla ya shule 24 zimefikiwa na mradi huu ambao pia umetoa mafunzo kwa walimu 40 wa shule na Wakunga wa jadi, makungwi/Nyakanga 34 wanaotoa elimu kwa wasichana wanaobalehe.

Pia alisisitiza kwamba elimu hii juu ya masuala ya hedhi itawezesha kuongeza uelewa wa jamii kwa ujumla juu ya umuhimu wa kuwasaidia wasichana ili waweze kuhudhuria masomo yao kwa ufanisi zaidi na kufikia malengo yao kimaisha.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Vodacom Foundation, Yessaya Mwakifulefule alisema kuwa
elimu inayotolewa na mradi na mradi huo utaliwezesha Taifa kupunguza kasi ya maambukizi ya
mgonjwa ya kujamiiana ikiwemo maambukizi ya Virusi vya vinavyosababisha Ukimwi (VVU),
miongoni mwa vijana.

Mwakifulefule alisema kila msichana atakuwa akipatiwa pakiti mbili za vifaa hivyo kwa mwezi na zoezi hili litafanyika kwa muda wa miezi mitano mfululizo.

“Tunajivunia kuwa sehemu ya chachu ya maendeleo katika sekta ya elimu hususani mradi huu wa
Hakuna Wasichoweza ambao umelenga kunufaisha jumla ya wasichana 6000 waliopo na wasiopo
shuleni”, alisema Mwakifulefule.

Naye Mtaalamu wa Masuala ya Misaada kwa jamii kutoka Vodafone, Laura Turkington alisema mradi
unakuza ushiriki wa wadau mbali mbali katika kukuza viwango vya elimu pamoja na kutoa taarifa
sahihi kwa jamii kuhusu changamoto zinazowakabili wasichana katika kipindi cha balehe.

Aidha, T-MARC imetoatoa shukurani kwa Shirika la USAID ambalo limetoa msaada wa dola za
Kimarekani laki mbili (200,000)  kufadhili uanzishwaji wa mradi huu pamoja na Vodacom
Foundation ambayo imechangia shilingi milioni 160, kufanikisha awamu hii ya kwanza ya mradi.




 Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara Bw. Salumu Masalanga (katikati) akipokea msaada wa pedi kwa niaba ya  wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Maendeleo chini ya programu ya Hakuna Wasichoweza iliyofadhiliwa na Vodacom na T-MARC.

Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara Bw. Salum Masalanga (katikati) akikabidhi msaada wa pedi kwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi ya Maendeleo, Neema Mohamed chini ya programu ya Hakuna Wasichoweza iliyofadhiliwa na Vodacom na T-MARC.

Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii Vodacom, Yesaya Mwakifulefule (kushoto) na Mratibu wa Mradi kutoka T-MARC Tanzania, Bi. Dorice Chalambo (wa pili kulia) kwa pamoja wakikabidhi msaada wa pedi kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Maendeleo chini ya programu ya Hakuna Wasichoweza iliyofadhiliwa na Vodacom na T-MARC.

UKAWA WALIVYOWASHA MOTO KISIWANI ZANZIBAR

VIONGOZI Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), jana walifanya mkutano wao wa kwanza katika eneo la Kibanda maiti, mjini Zanzibar.




MWANASIASA MAARUFU WA CHAMA CHA SINN FEIN, GERRY ADAMS, AKAMATWA KASKAZINI IRELAND.


JESHI la Polisi nchini Kazkazini Ireland wamemkamata mwanasiasa mashuhuri wa chama

cha Sinn Fein, Gerry Adams kwa kuhusishwa na mauaji yaliyotokea zaidi ya miaka 40 iliyopita.

Adams anahojiwa kuhusu mauaji ya Jean McConville ambaye alitekwanyara na kundi la waasi

la IRA mnamo mwaka 1972 na kisha akapatikana amepigwa risasi na kuuawa .

Kiongozi huyo amekanusha kuhusika kivyovyote vile akisema kuwa alijipeleka binafsi kuzungumza na

polisi ilikujaribu kusuluhisha madai hayo yaliyomwandama kwa miaka mingi mno .

Adams anakanusha kuhusika kwa vyovyote vile na utekaji nyara wala mauaji yake bi Mc Conville

ambaye alikuwa mama wa watoto 10 .Madai hayo yanafwatia mahojiano mjini Belfast

mwaka wa 2001-2006 baina ya chuo kikuu cha Boston Marekani na wakereketwa wa vita hivyo

vilivyonuiwa kuikomboa Ireland kutoka kwenye minyororo ya ukoloni.

Mahojiano hayo yalifanywa kwa misingi kuwa yangewekwa siri hadi baada ya vifo vya wahusika

wakuu, lakini baada ya kesi za kutaka kutambulika wahusika na wahasiriwa waliotoweka wakati wa

vita hivyochuo hicho kililazimishwa kutoa sehemu ya mahojiano kwa serikali ya Ireland.

Mmoja kati ya watu 16 waliosemekana kutoweka ni Mc Conville, hata hivyo mjane huyo alilaumiwa na

IRA kuwa mpelelezi wa polisi lakini baada ya ufafanuzi wa polisi yapata mwaka wa 1999, ambapo

McConville ilibainika hakuwa.Kundi hilo la IRA lilikiri kutekeleza mauaji yake bi

McConville mwaka wa 1999 lakini mwili wake ulipatikana mwaka wa 2003 ukiwa umetupwa

kwenye ufukwe wa bahari.IRA inashtumiwa kwa kampeini na mauaji

yaliyotikisa Ireland kaskazini kwa takriban miaka 30.

Chanzo: BBC SWAHILI.

Jumatano, 30 Aprili 2014

BARABARA YA UHURU SASA SAFI.

Mambo safi kwa vyombo vya moto.
Daradara ikipita katika barabara ya uhuru, baada nyia hiyo kukarabatiwa leo eneo la Shule ya Uhuru Mchanganyiko, jijini Dar es Salaam.

Jumamosi, 7 Desemba 2013

HAYA NI CHADEMA LINDI

Mwenyekiti aliyejiuzuru CHADEMA Mkoa wa Lindi Ally Chitanda amemjibu katibu Mkuu wa Chama hicho Dk. Wilbrod Slaa na kumwita ni mwenye tama na mbinafsi huku chama kikitafunwa na udini, ukabila na ukanda.

Chitanda alitoa taarifa kwa vyombo vya habari jana, Dar es Salaam, ambapo alisema kuhusu hoja hiyo ya udini, ukabila na ukanda ni kwamba kati ya wakurugenzi sita, watatu ni wenyeji wa Mkoa wa Kilimanjaro na wote sita hakuna hata Mwislamu.

Alisema watanzania kutambua kuwa Dk. Slaa ni mlevi wa madaraka  na ndio maana hata yeye aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkoa, Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa na Katibu wa Sekretarieti anamwita mtu mdogo katika chama.

“Ikiwa mimi ananiita mtu mdogo na nyazifa zangu hizo kwenye chama je, wanachama wa kawaida atawaitaje? Mimi nawathibitishia watanzania wenzangu mungu alitunusuru 2010, uchaguzi uliopita kwani Dk. Slaa ni mbinafsi na anatamaa.” Alisema Chitanda.

Akizungumzia kuhusu uhasama ulipo kati ya Zitto na Mwenyekiti Freeman Mbowe na Dk. Slaa, Chitanda alisema ulitokana na  Zitto kutaka kugombea uenyekiti wa chama hicho mwaka 2009.

Alisema uhasama huo uliongezeka baada ya Mbowe na Dk. Slaa kuwakumbatia watu ambao walikuwa wakimtukana Zitto, kwenye mitandao ya kijamii.

“Nasema Zitto hana kosa lolote linalofanana na adhabu aliyopewa na  chama hicho, hivyo Mbowe na Dk. Slaa wanajukumu la wajibu wa kusimamia haki na ukweli ndani ya CHADEMA.” Alisema Chitanda.

Aidha, Chitanda alizungumzia kuhusu hoja iliyotolewa na msemaji wa CHADEMA, Makene iliyomtaka aonyeshe barua ya uteuzi wa Katibu wa Sekretarieti alisema hoja hiyo inaonyesha ni namna Dk. Slaa alivyokuwa dhaifu katika utendaji wake wakazi.

Alisema nafasi hiyo alipewa mwaka 2010 na ilitokana na aliyetakiwa kufanya kazi hiyo ni Zitto, hivyo kutokana na kukabiliwa na majukumu mengi ya kikazi, akapendekezwa yeye atiuliwe kushika wadhifa huo ambapo sekretarieti ilithibitisha uteuzi huo chini ya uenyekiti wa Dk. Slaa.

“Uthibitisho wa kutosha ninao wa kuitumikia nafasi hiyo na ninayo baadhi ya maelekezo niliyokuwa nikipewa na Dk. Slaa na endapo sikua na wadhifa huo kwenye vikao vya sekretarieti, Kamati Kuu nilikuwa naingia kufanya nini?” alisema.